Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Judith Kapinga, ametembelea Banda la Ofisi ya Rais – Maendeleo ya Vijana katika Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba), ambapo amejionea huduma mbalimbali zinazotolewa na Ofisi hiyo pamoja na maonesho ya bidhaa kutoka kwa wajasiriamali waliowezeshwa kupitia programu za Serikali.
Katika ziara hiyo, Mhe. Kapinga amepatiwa maelezo kuhusu huduma zinazotolewa katika banda hilo, zikiwemo Elimu ya masuala ya sheria, Elimu ya uzalendo, huduma za Mfumo wa Youth Empowerment System (YES) pamoja na fursa mbalimbali zinazoratibiwa na Ofisi ya Rais – Maendeleo ya Vijana kwa ajili ya kuwawezesha wananchi, hususan vijana.
Mhe. Kapinga amepongeza juhudi zinazofanywa na Ofisi ya Rais – Maendeleo ya Vijana katika kusogeza huduma karibu na wananchi kupitia maonesho hayo. Pia amewapongeza wajasiriamali waliowezeshwa na Serikali kwa ubunifu wao na matumizi mazuri ya fursa walizopata, huku akihimiza wananchi kuendelea kutembelea banda hilo ili kupata elimu na huduma mbalimbali zinazotolewa.
- "Huduma bora: Mafunzo ya NeST Morogoro yaiweka Ofisi ya...
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Maendeleo ya Vijana, Mhe. Joel Nanauka, ak...
- Makundi maalumu ikiwemo Vijana waaswa kujiunga NeST kupata fursa ya 30% ya Zab...
- Huduma bora kwa watanzania, NeST kutoa fursa kwa wazabuni wa...
Serikali imekabidhi pikipiki 22 zenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 87 kw...