Ofisi ya Rais
Maendeleo ya Vijana
WANANCHI WAHUDUMIWE KWA WELEDI: NAIBU KATIBU MKUU...

WANANCHI WAHUDUMIWE KWA WELEDI: NAIBU KATIBU MKUU OR – VIJANA

17 Jun, 2026
WANANCHI WAHUDUMIWE KWA WELEDI: NAIBU KATIBU MKUU OR – VIJANA

Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais - Maendeleo ya Vijana, Dkt. Kedmon Mapana leo Juni 17, 2026 ametembelea banda la Ofisi hiyo kwenye Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma, Chinangali Park, Dodoma.

Dkt. Mapana amezungumza na Watumishi wa ofisi hiyo kujua utayari wao katika kutoa huduma kwa wananachi hususani vijana wanaofika katika banda hilo kutaka huduma za kiutumishi.

Akiwa bandani hapo ametoa maelekezo kwa watumishi wa Ofisi hiyo kutoa huduma kwa weledi, ili kuakisi kaulimbiu ya maadhimisho hayo inayosema "kuchochea uwajibikaji jumuishi kwa huduma endelevu."