Ofisi ya Rais
Maendeleo ya Vijana
WAZIRI NANAUKA AVUTIWA NA KIWANDA CHA VIJANA MISSE...

WAZIRI NANAUKA AVUTIWA NA KIWANDA CHA VIJANA MISSENYI, APONGEZA MATOKEO YA MKOPO WA ASILIMIA 10%

21 Mar, 2026
WAZIRI NANAUKA AVUTIWA NA KIWANDA CHA VIJANA MISSENYI, APONGEZA MATOKEO YA MKOPO WA ASILIMIA 10%

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Maendeleo ya Vijana, Mheshimiwa Joel Arthur Nanauka, ametembelea Kiwanda cha Missenyi Standard Chalks, ambacho ni kiwanda cha vijana kilichopo Wilaya ya Missenyi, Kata ya Mutukula. 

Katika ziara hiyo, Mheshimiwa Waziri alikagua shughuli za uzalishaji na kujionea maendeleo ya kiwanda hicho kinachoendeshwa na vijana, ambacho ni miongoni mwa wanufaika wa mkopo wa asilimia kumi (10%) ya Halmashauri. Mradi huo umewezesha vijana kuongeza uzalishaji, kuunda ajira na kuchangia ukuaji wa uchumi wa eneo hilo. 

Mheshimiwa Nanauka alipongeza juhudi za vijana hao na kusisitiza kuwa Serikali itaendelea kuwekeza katika kuwawezesha vijana kiuchumi kupitia mikopo na fursa mbalimbali, ili kukuza ujasiriamali na maendeleo endelevu ya taifa.