Naibu katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Maendeleo ya Vijana Dkt. Kedmon Elisha Mapana amewataka vijana kuchangamkia fursa zinazotolewa na serikali kupitia Wizara ya Maendeleo ya Vijana, kwa lengo la kuwawezesha kuwa Daraja la maendeleo ya taifa.
Hayo yamesemwa wakati wa uzinduzi wa Jukwaa la Vijana “Vijana Platform” katika Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni, ambapo pia Dkt. Mapana ameeleza kuwa Wizara ya Maendeleo ya Vijana imeendelea kuweka mikakati ya kushugulikia masuala ya vijana ikiwemo kuanzisha Idara nne zitakazojihusisha na vijana moja kwa moja.
Vilevile, Dkt. Mapana amesema kuwa, kuanzishwa kwa Vijana Platform kunalenga kuwawezesha vijana kiuchumi, kuwapa nafasi ya kuchangia mawazo yao, kuwezesha kuundwa kwa baraza la vijana, kuwezesha vijana kuwa na taarifa sahihi kuhusu fursa za vijana zinazotolewa na serikali kupitia taasisi zake mbalimbali ikiwemo kupitia PPRA.
Kadhalika, Dkt. Mapana amewataka vijana kutumia shindano la ‘Vijana Uchumi Challenge’ kuwasilisha mawazo yao yatakayoleta suluhu ya changamoto mbalimbali zinazoikabili jamii katika nyanja mbalimbali.
Aidha, amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuanzisha Wizara ya Vijana ili kuratibu masuala ya vijana na kutatua changamoto zao kwa ufanisi zaidi.
Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni Mhe. Songoro H. Mnyonge am...
Mkuu wa Wilaya ya Ubungo, Mhe. Albert Gasper Msando ameongoza uzinduzi wa Jukwaa...
-Vijana waapa kudumisha uzalendo,Kuulinda Mwenge -Waziri Nanauka azidi ku...
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Maendeleo ya Vijana Mhe. Joel Arthur Nanauka, ame...
-Rais Samia azindua minara 758 kuimarisha Mawasiliano Na Byarugaba Inno...