Ofisi ya Rais
Maendeleo ya Vijana
BRELA YATOA ELIMU YA URASIMISHAJI WA BIASHARA KWA...

BRELA YATOA ELIMU YA URASIMISHAJI WA BIASHARA KWA VIJANA KATIKA BANDA LA OFISI YA RAIS – MAENDELEO YA VIJANA SABASABA

01 Jul, 2026
BRELA YATOA ELIMU YA URASIMISHAJI WA BIASHARA KWA VIJANA KATIKA BANDA LA OFISI YA RAIS – MAENDELEO YA VIJANA SABASABA

Mamlaka ya Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) imetembelea Banda la Ofisi ya Rais – Maendeleo ya Vijana katika Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba) na kutoa elimu kwa vijana wajasiriamali kuhusu umuhimu wa kurasimisha biashara zao.

Akizungumza wakati wa ziara hiyo, Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano wa BRELA, Theresa Chilambo, amesema wamevutiwa na ubunifu wa vijana wanaoshiriki maoneshoni, lakini akasisitiza kuwa bado wapo ambao hawajasajili biashara zao, jambo linaloweza kuwanyima fursa ya kukuza biashara hadi kuwa kampuni.
Ameongeza kuwa BRELA ina jukumu la kusajili na kurasimisha biashara, kutoa leseni pamoja na kulinda majina ya biashara na chapa (brandi), hatua inayowasaidia wajasiriamali kulinda ubunifu wao dhidi ya matumizi yasiyo halali.

Bi. Chilambo aliongeza kuwa biashara isiposajiliwa inaweza kuchukuliwa na mtu mwingine akaisajili, hali inayoweza kumfanya mmiliki halisi kupoteza haki ya kuitambulisha rasmi.